Matusi ni silaha sawa na zilivyo silaha nyingine za kupambana na adui,
lakini silaha hii haijafua dafu kwa Lowassa. Wanaompenda Lowassa
hawakatishwi na matusi kwa Lowassa. Wanaompenda Lowassa na UKAWA
wanaposikia matusi dhidi ya Lowassa na UKAWA wanajihisi kama vile
wametukanwa wao pia. Hivyo, wanapambana na matusi hayo kwa njia
mbalimbali kama vile kuzidisha mahaba kwa Lowassa, kuhudhuria mikutano
yake, kukaa kimya bila kuyajibu, kuzima na kususia vyombo vya habari
(redio, tv na magazeti) vinayotumika kupeperusha matusi hayo, kuongeza
zaidi mbinu za kampeni na hatimaye kujiandikisha na kwenda kupiga kura
kwa wingi. Baada ya matusi kushindwa kufanya kazi yake iliyokusudiwa kwa
Lowassa mbinu gani mpya itafuata?
Tagged with: SIASA
Hakuna maoni :