BAADA ya kuzichapa Man United, Watford na Bayern Munich, Jumamosi Arsenal wana nafasi ya kutwaa uongozi wa Ligi Kuu England kwa mara ya kwanza katika Miaka Miwili ikiwa wataifunga Evrton Uwanjani Emirates.
Msimu uliopita kwenye Mechi kama hii, Arsenal iliifunga Everton 2-0 na safari hii Arsenal wapo kwenye wimbi zuri la ushindi wakitoka kuzichapa 3-0 Man United na Watford kwenye Ligi na 2-0 Bayern Munich kwenye UEFA CHAMPIONZ LIGI.
Everton wao wanatinga kwenye Mechi hii wakitoka kwenye kipigo cha 3-0 Nyumbani kwao Goodison Park kutoka kwa Man United.
Ikiwa Arsenal wataifunga Everton basi watakaa kileleni mwa Ligi pengine hadi Jumapili wakati Dabi ya Manchester ikichezwa huko Old Trafford kati ya Man United na Man City ambao wana nafasi ya kuishusha Arsenal toka kileleni.
Majeruhi:
-Arsenal: Ospina, Ramsey, Rosicky, Wilshere, Welbeck
-Everton: Besic, Baines, Hibbert, Pienaar
VIKOSI:
REFA: Lee Mason
LIGI KUU ENGLAND
RATIBA:
**Saa za Bongo
Jumamosi Oktoba 24
1700 Aston Villa v Swansea
1700 Leicester v Crystal Palace
1700 Norwich v West Brom
1700 Stoke v Watford
1700 West Ham v Chelsea
1930 Arsenal v Everton
Jumapili Oktoba 25
1500 Sunderland v Newcastle
1705 Bournemouth v Tottenham
1705 Man United v Man City
1915 Liverpool v Southampton
Hakuna maoni :