SIASA

SIASA

MAONI

MAONI

BURUDANI

MICHEZO

/ / HABARI MPYA KUMHUSU MBWANA SAMATTA NA TUZO YA MWANASOKA BORA WA AFRIKA





MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta ameingia tatu bora ya Tuzo ya Mwanasoka Bora anayecheza soka la ndani barani Afrika.

Tovuti ya Shirikisho la Soka Afrika imesema Samatta ameingia fainali na kipa Robert Kidiaba anayecheza naye TP Mazembe ya DRC na Baghdad Boundjah wa Algeria na Etoile du Sahel ya Tunisa.
Katika tuzo ya Mwanasoka Bora wa Jumla wa Afrika, walioingia fainali ni Andre Ayew wa Ghana na Swansea City, Pierre-Emerick Aubameyang wa Gabon na Borussia Dortmund na Yaya Toure wa Ivory Coast na Manchester City, anayeshikilia tuzo hiyo.



Majina hayo yametangazwa mchana wa leo katika Mkutano na Waandishi wa Habari mjini Abuja, Nigeria na washindi watapatikana kutokana na kura zitakazopigwa na makocha wakuu wa timu za taifa au Wakurugenzi wa Ufundi wa Vyama na mashirikisho ya soka ya nchi zote wanachama wa CAF.

Washindi watatangazwa katika usiku wa tuzo za Glo-CAF Januari 7 mwaka 2016.

«
Next

Chapisho Jipya

»
Previous

Taarifa za zamani

About Unknown

Asante kwa kutembelea SELASINI HABARI,NITAKUHABARISHA, KUKUELIMISHA NA KUKUBURUDISHA HIVYO USIKOSE KUTEMBELEA SELASINIHABARI.BLOGSPOT.COM.

Hakuna maoni :

Leave a Reply