MOROCCO |
Kocha Hemed Morocco huenda asijiunge tena na Simba baada ya suala lake kuingia figisu.
Hali
hiyo inatokana na kocha huyo kuamua kutosaini mkataba kama walivyokuwa
wamekubaliana baada ya kugundua mshahara wake ulikuwa umepunguzwa.
“Kweli
tulikuwa tumekubaliana kila kitu, nilisafiri kutoka Zanzibar kuja hapa
Dar es Salaam kwa ajili ya kumalizana na kusaini mkataba. Hii ilikuwa
hivi baada ya kuwa tumeanza mazungumzo kule Zanzibar.
“Lakini
ajabu nimekuja kuona mkataba umebadilishwa na kuna vipengele havipo
sawa, sasa naona haitakuwa kama nilivyotarajia,” alisema.
Ingawa
Morocco amekuwa akificha kuhusiana na suala hilo, lakini kipengele
kilichobadilishwa ni cha mshahara na inaonekana kocha huyo msaidizi wa
Taifa Stars hatakubali.
Kama itakuwa hivyo, Simba itaendelea kusaka kocha mwingine na inawezekana akawa anatokea nje ya Tanzania.
Hakuna maoni :