Hoteli ya Kilimanjaro Kempinski ni moja ya hoteli bora kabisa ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.
Kawaida
zimekuwa zikifikia timu za taifa za Ivory Coast, Misri na nyinginezo.
Kwa upande wa timu Al Ahly ya Misri, mara kadhaa wamekuwa wakikataa
kufikia hoteli walizopangiwa na Yanga au Simba na kwenda kukaa pale.
Katika
hoteli hiyo yenye mazingira mwanana kila eneo, kawaida chumba ni
kuanzia dola 248 (zaidi ya Sh 520,800) kwa siku. Safari hii, Yanga ndiyo
walikuwa hapo.
Yanga
walifikia kwenye hoteli hiyo na kuishi kwa siku moja, kabla ya kwenda
na kuimaliza Simba kwa kuichapa kwa mabao 2-0 kwenye Uwanja wa Taifa na
kurejea kileleni.
Yanga
walitua Kempinski wakiwa wanatokea Pemba ambako pia waliishi katika
mazingira ya kitalii kabla ya kurejea Dar es Salaam tayari kwa mechi
dhidi ya watani wao.






Hakuna maoni :