SIASA

SIASA

MAONI

MAONI

BURUDANI

MICHEZO

/ / AZAM FC WAREJEA DAR KUISUBIRI MBEYA CITY, PATASHIKA LITAKUWA CHAMAZI JUMAPILI HII



MECHI ZIJAZO LIGI KUU YA VODACOM TZ BARA

Jumamosi Septemba 26, 2015
Simba SC Vs Yanga SC
Coastal Union Vs Mwadui FC
Prisons FC Vs Mgambo JKT
JKT Ruvu Vs Stand United
Mtibwa Sugar Vs Majimaji FC
Kagera Sugar Vs Toto Africans
Septemba 27, 2015
African Sports Vs Ndanda FC
Azam FC Vs Mbeya City 
Azam FC watakuwa wenyeji wa Mbeya City katika mchezo ujao wa Ligi Kuu 

AZAM FC imerejea jana usiku Dar es Salaam kutoka Shinyanga ambako ilifanikiwa kuvuna pointi sita katika mechi za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
Baada ya ushindi wa 2-0 dhidi ya Stand United na 1-0 dhidi ya Mwadui FC, Azam FC imetua kwa ndege usiku wa jana Dar es Salaam kwa maandalizi ya mchezo ujao dhidi ya Mbeya City.
Mabingwa hao wa Afrika Mashariki na Kati watakuwa wenyeji wa Mbeya City katika mfululizo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
Azam FC imeshinda mechi zote tatu za mwanzo za Ligi Kuu, dhidi ya Prisons 2-1 Chamazi na hizo za Shinyanga, ikiwa inababana mbavu na vigogo, Simba na Yanga SC kileleni.
Mechi za Azam FC inayodhaminiwa na benki ya NMB na Mbeya City inayodhaminiwa na RB Battery za Bin Slum Company Limited, zimekuwa kali na za kusisimua popote zinapokutana timu hizo, iwe Mbeya au Chamazi na Jumapili inatarajiwa patashika nyingine.

«
Next

Chapisho Jipya

»
Previous

Taarifa za zamani

About Unknown

Asante kwa kutembelea SELASINI HABARI,NITAKUHABARISHA, KUKUELIMISHA NA KUKUBURUDISHA HIVYO USIKOSE KUTEMBELEA SELASINIHABARI.BLOGSPOT.COM.

Hakuna maoni :

Leave a Reply