SIASA

SIASA

MAONI

MAONI

BURUDANI

MICHEZO

/ / MESSI AFUTIWA KESI ILA BABAKE HATARINI KIFUNGO!





MESSIMamlaka za uendeshaji Kesi huko Spain zimeamua kumfutia Mashitaka Lionel Messi ya ukwepaji Kodi.
Mamlaka hizo zimetoa uamuzi huo baada ya kuafiki hoja kwamba wakati makosa hayo yakitendeka Messi alikuwa na umri mdogo kiasi cha kutojua nini kinaendelea.
Hata hivyo Kesi hiyo itaendelea kwa Baba yake Messi aitwae Jorge Messi.
Messi, ambae ni Mchezaji wa Barcelona, alishtakiwa yeye pamoja na Baba yake kwa ukwepaji Kodi kati ya 2007 na 2009 unaokadiriwa kufikia Euro Milioni 4.1.
Ukwepaji huo wa Kodi ni ule wa kuuza Haki za Matangazo ya Staa huyo nje ya Spain na hivyo kuikosesha Nchi hiyo mapato.
Licha ya kumfutia Mashitaka Messi, Waendesha Mashitaka wa Kesi hiyo wamesema Messi huenda akaitwa Mahakamani kutoa ushahidi dhidi ya Baba yake ambae ndie Wakala wake tangu aanze Soka.
Ikiwa atapatikana na hatia, Jorge Messi anaweza kufungwa Miezi 18 au kupigwa Faini Euro Milioni 2 au vyote kwa pamoja.
Hata hivyo, mara baada ya tuhuma hizi kuibuka Messi na Baba yake walilipa Kodi yote waliyokuwa wakidaiwa pamoja na malimbikizo ya Riba yake.

«
Next

Chapisho Jipya

»
Previous

Taarifa za zamani

About Unknown

Asante kwa kutembelea SELASINI HABARI,NITAKUHABARISHA, KUKUELIMISHA NA KUKUBURUDISHA HIVYO USIKOSE KUTEMBELEA SELASINIHABARI.BLOGSPOT.COM.

Hakuna maoni :

Leave a Reply