SIASA

SIASA

MAONI

MAONI

BURUDANI

MICHEZO

/ / MEXICO YAITUPA USA NA KUTINGA FIFA KOMBE LA MABARA URUSI 2017!


Mexico3Usa2Bao la Paul Aguilar katika Dakika ya 118 ndani ya Dakika za Nyongeza 30 limewapa Mexico ushindi wa Bao 3-2 na kutinga kwenye Mashindano ya FIFA ya Kombe la Mabara yatakayochezwa huko Russia Mwaka 2017.
 
Kwenye Mechi hiyo iliyochezwa Alfajiri ya Leo huko Rose Bowl, Pasadena, USA, mbele ya Watu 93,723, Mexico walianza kufunga kwa Bao la Dakika ya 10 la Javier Hernandez 'Chicharito' na USA kusawazisha Dakika ya 15 kupitia Geoff Cameron.
 
Bao hizo zilidumu hadi Dakika 90 kwisha na ndipo Dakika za Nyongeza 30 zikachezwa na Mexico kuibwaga USA kwa mara ya kwanza katika Mechi 7 walizokutana chini ya Kocha wa USA Jurgen Klinsmann.
===============
MAGOLI:
USA 2
-Geoff Cameron Dakika ya 15
-Bobby Wood 108
MEXICO 3
-Chicharito Dakika ya 10
-Oribe Peralta 96
-Paul Aguikar 118
===============
Mechi hii ilizikutanisha Washindi waliopita wa Mashindano ya CONCAFA CUP ili kupata Timu moja kuwakilisha Bara hili la FIFA la Nchi za Marekani ya Kati na Kaskazini na Nchi za Visiwa vya Carribean ili kucheza Mashindano ya FIFA ya Kombe la Mabara huko Russia Mwaka 2017.
 
Kombe la Mabara huchezwa Mwaka mmoja kabla ya Fainali za Kombe la Dunia na kwa vile Fainali zijazo zitachezwa Russia Mwaka 2018 Kombe hili litachezwa huko huko Russia kuanzia Tarehe 17 Juni 2017 hadi Julai 2, 2017.
 
Washiriki wa Kombe la Mabara 2017 ni Wenyeji Russia, Mabingwa wa Dunia Germany, Mexico na Wawakilishi wengine Watano toka Mabara mengine ya FIFA kama vile CAF, AFC, OFC, CONMEBOL na UEFA.

«
Next

Chapisho Jipya

»
Previous

Taarifa za zamani

About Unknown

Asante kwa kutembelea SELASINI HABARI,NITAKUHABARISHA, KUKUELIMISHA NA KUKUBURUDISHA HIVYO USIKOSE KUTEMBELEA SELASINIHABARI.BLOGSPOT.COM.

Hakuna maoni :

Leave a Reply