Jose
Mourinho atajua nini litamkuta baada ya Siku chache kutoka kwa FA,
Chama cha Soka England, baada ya Jana kupewa Kadi Nyekundu wakati Timu
yake Chelsea ikifungwa 2-1 na West Ham huko Upton Park.
Mourinho aliadhibiw na Refa Jon Moss wakati wa Haftaimu baada ya
kudaiwa kutaka 'kuvamia' Chumba cha Waamuzi' wakati wa Mapumziko.
Wakati huo Chelsea ilishafungwa 1-0 na West Ham na kubaki Mtu baada
ya Kiungo wao Nemanja Matic kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu baada ya
Kadi za Njano 2 na pia Msaidizi wa Mourinho, Silvino Louro, kumfuatia
Matic nje baada nae kupewa Kadi Nyekundu alipolalamika.
Katika Miezi ya hivi karibuni, Mourinho amekuwa akilalamika kuhusu yeye na Timu yake kusakamwa na Marefa.
Kauli hizo zilimfanya FA impige Faini Pauni 50,000 na kumpa Kifungo
cha Mechi 1 asikanyage Uwanjani lakini Kifungo hicho kimesimamishwa kwa
Mwaka Mmoja hadi Tarehe 16 Oktoba 2016 ili kumwangalia mwenendo wake.
Kutokana na Kadi Nyekundu ya Jana sasa FA watasubiri Ripoti ya Refa
Jon Moss na kisha kuamua kama hili linastahili kumrejeshea Kifungo
chake na Adhabu nyingine stahiki.
Vile vile, Mourinho Jana aligoma kuongea na Wanahabari baada ya
Mechi ikiwa ni kinyume na Sheria za Ligi Kuu England lakini kwa kosa
hili Klabu ndio hupigwa Faini.
Msimu huu, Chelsea, ambao ndio Mabingwa Watetezi, wameshafungwa Mechi 5 kati ya 10 za Ligi na wapo Nafasi ya 15.
Hakuna maoni :