Taifa Stars imepoteza mechi yake dhidi ya Malawi kwa kufungwa bao
1-0 mjini Blantyre, lakini imesonga mbele katika mechi hizo za awali kuwania
kucheza Kombe la Dunia mwaka 2018 nchini Urusi.
Jijini Dar es Salaam, Jumatano.
Malawi
ilipata bao lake mwishoni mwa kipindi cha kwanza kupitia shuti kali la John
Banda lililombabatiza Kelvin Yondani na kumshinda kipa Ally Mustapha.
Hata hivyo
kipa huyo aliendelea kuwa shujaa kwa kuokoa michomo mingi katika kipindi cha
kwanza ambacho Malawi walikuwa vizuri zaidi.
Stars
walitumia muda mwingi kukaba hasa katika kipindi cha kwanza, angalau katika
kipindi cha pili wakaanza kuonyesha mabadiliko kwa kupambana zaidi.
Kutokana na ushindi huo, Stars inatarajia kucheza mechi mbili dhidi ya Algeria ambazo zitachezwa kati ya Novemba 9 na 17.
Hakuna maoni :