SIASA

SIASA

MAONI

MAONI

BURUDANI

MICHEZO

/ / WATANZANIA WAOMBWA KUJITOKEZA KUICHANGIA TAIFA STARS IIMALIZE ALGERIA



 Mwenyekiti wa Kamati ya kuisaidia Taifa Stars, Farouk Baghouza amewaomba Watanzania kujitokeza na kuichangia kamati yake ili iweze kufanikisha lengo la kuisaidia Stars.

Akizungumza leo na waandishi wa habari, pamoja na kutangaza kamati kubwa na ndogondogo kwa ajili ya kuisaidia Stars, Farouk alisisitiza suala la Watanzania kujitolea.
“Mwenye maji, mwenye dawa tunakaribisha michango. Lengo ni kuisaidia timu, lakini lengo ni kuonyesha umoja na utaifa wetu.
“Taifa Stars inatuwakilisha Watanzania wote hata wasio wapenda soka, tafadhari tuungane pamoja katika kipindi hiki kuhakiksha tunaing’oa Algeria,” alisema.
Stars inakutana na Algeria Novemba 14 katika mechi ya kwanza iatakayochezwa jijini Dar es Salaam kabla ya kurudiana Novemba 17 nchini Algeria.
Mechi hiyo ni ya kuwania kucheza Kombe la Dunia nchini Urusi mwaka 2018.
Stars imepata nafasi hiyo baada ya kuing’oa Malawi kwa jumla ya mabao 2-1 ikiwa imeanza na ushindi wa mabao 2-0 jijini Dar es Salaam, ikapoteza 1-0 mjini Blantyre.
Algeria ndiyo timu bora kuliko zote Afrika, pia ndiyo timu ya Afrika iliyofanya vizuri zaidi katika michuano ya kwanza ya Kombe la Dunia nchini Brazil, mwaka jana.

«
Next

Chapisho Jipya

»
Previous

Taarifa za zamani

About Unknown

Asante kwa kutembelea SELASINI HABARI,NITAKUHABARISHA, KUKUELIMISHA NA KUKUBURUDISHA HIVYO USIKOSE KUTEMBELEA SELASINIHABARI.BLOGSPOT.COM.

Hakuna maoni :

Leave a Reply