SIASA

SIASA

MAONI

MAONI

BURUDANI

MICHEZO

/ / IJUMAA SPAIN-ENGLAND, KEPTENI ROONEY BENCHI MECHI HII


ROONEY-ENGLANDMENEJA wa England Roy Hodgson ametangaza kwamba Wayne Rooney hataanza kwenye Mechi ya Kirafiki na Spain ya Ijumaa huko Alicante Nchini Spain.

Mbali ya kutamka hilo, Hodgson pia amedokeza kuwa Mfungaji Bora wa Ligi Kuu England, Jamie Vardy, pia yupo mashakani kucheza Mechi hiyo kutokana na maumivu.

Hata hivyo, Hodgson amesisitiza kutoanza Mechi hiyo kwa Rooney ni kwa sababu tu anataka kuwapa nafasi Wachezaji wengine kuonyesha uwezo wao kabla hajateua Kikosi chake cha kucheza Fainali za EURO 2016 Mwezi Juni huko France.

Hodgson ametoboa kuwa Rooney ataanza Mechi ya Kirafiki ya Jumanne dhidi ya France Uwanjani Wembley Jijini London.

Akiongea na Wanahabari, Hodgson amesema: “Wayne yupo na mimi hii Leo kwa sababu ndie Kepteni wangu. Ni Mtu muhimu lakini hataanza Mechi ya Kesho. Tunaangalia Wachezaji wengine lakini ataanza Mechi na France Jumanne.”

Nae Rooney amekiri umuhimu wa kubadili Wachezaji kwenye Kikosi ili Meneja apate kupima kila Mchezaji.

Kuhusu Jamie Vardy ambae amepiga Bao katika Mechi zake 9 zilizopita za Ligi Kuu England anasumbuliwa na maumivu baada ya kuumia kwenye Mechi ya Jumamosi iliyopita Timu yake Leicester City ilipoifunga Watford.

Wikiendi hii, mbali ya hii ya Spain na England, zipo Mechi za Kimataifa za Kirafiki huku kadhaa zikiwa Bigi Mechi kama vile France v Germany, Belgium v Italy, England v France, Belgium v Spain na Germany v Netherlands ambazo zitapigwa Ijumaa na Jumanne.
KIMATAIFA KIRAFIKI
Ratiba
*Saa za Bongo
Jumatano Novemba 11
15:00 Jordan v Malta                 
20:00 Estonia v Georgia             
Alhamisi Novemba 12         
17:00 Oman v New Zealand                 
19:00 Macedonia v Montenegro            
20:00 Andorra v Saint Kitts And Nevis            
Ijumaa Novemba 13        
3:00   Solomon Islands v Fiji                
20:30 Qatar v Turkey                 
21:00 Luxembourg v Greece                 
21:45 Poland v Iceland              
21:45 Northern Ireland v Latvia            
21:45 Belgium v Italy                 
21:45 Portugal v Russia              
22:30 Czech Republic v Serbia              
22:45 Spain v England               
22:45 Slovakia v Switzerland                
22:45 Wales v Netherlands                  
23:00 France v Germany            
Jumamosi Novemba 14         
10:00 Hong Kong v Macau
Jumanne Novemba 17
Tuesday 17 Nov 2015         
3:00   Italy v Poland                   
3:00   Lebanon v New Zealand              
14:00 Macedonia v Lebanon                 
18:00 Russia v Croatia               
19:00 Estonia v Saint Kitts And Nevis             
19:00 Azerbaijan v Moldova                 
20:15 Turkey v Greece               
21:30 Luxembourg v Portugal               
21:45 Austria v Switzerland                  
21:45 Poland v Czech Republic             
21:45 Slovakia v Iceland            
21:45 Belgium v Spain               
22:00 England v France              
22:45 Germany v Netherlands              
22:45 Italy v Romania

«
Next

Chapisho Jipya

»
Previous

Taarifa za zamani

About Unknown

Asante kwa kutembelea SELASINI HABARI,NITAKUHABARISHA, KUKUELIMISHA NA KUKUBURUDISHA HIVYO USIKOSE KUTEMBELEA SELASINIHABARI.BLOGSPOT.COM.

Hakuna maoni :

Leave a Reply