MATOLA |
Licha ya
Selemani Matola kuondoka ndani ya kikosi cha Simba siku za hivi karibuni, kocha mkuu wa timu
hiy, Dylan Kerr amempongeza kwa kupata timu nyingine.
Matola
alibwaga manyanga ndani ya kikosi hicho baada ya kudai kuwa wamekuwa
hawaelewani na Kerr, kwa sasa ni kocha mkuu wa Geita Gold Sport ya Ligi Daraja
la Kwanza.
KERR, MATOLA NA IDDI SALIM. |
Kerr alisema: “Nilikuwa sifahamu kama
amefanikiwa kupata timu nnyingine, ndiyo mnaniambia sasa lakini siyo kitu
kibaya na mpongeza ni jambo zuri ingawa mimi na yeye hatujawahi kuwasiliana
hata siku moja tangu aondoke hapa klabuni."
Matola
ambaye ni nahodha wa zamani wa Simba, aliondoka Simba akidai Kerr
alikuwa hasikilizi ushauri wake au kumpa ushirikiano wa kutosha.
Hakuna maoni :