RATIBA KOMBE LA CHALLENGE 2015
Leo; Novemba 25, 2015
Kenya Vs Burundi
Somalia Vs Ethiopia
Malawi v Djibouti
S. Sudan v Sudan
Ijumaa Novemba 27, 2015
Rwanda Vs Somalia
Zanzibar Vs Kenya
S. Sudan v Malawi
Djibouti V Sudan
Uganda Vs Burundi
Tanzania Vs Ethiopia
NAHODHA wa Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars, John Raphael Bocco amesema kwamba wanafahamu wana deni kubwa kwa Watanzania, hivyo wataendelea kujitahidi wafanye vizuri katika michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge inayoendelea nchini Ethiopia.
Somalia Vs Ethiopia
Malawi v Djibouti
S. Sudan v Sudan
Ijumaa Novemba 27, 2015
Rwanda Vs Somalia
Zanzibar Vs Kenya
S. Sudan v Malawi
Djibouti V Sudan
Uganda Vs Burundi
Tanzania Vs Ethiopia
Nahodha wa Kilimanjaro Stars, John Bocco amesema wana deni kwa Watanzania |
NAHODHA wa Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars, John Raphael Bocco amesema kwamba wanafahamu wana deni kubwa kwa Watanzania, hivyo wataendelea kujitahidi wafanye vizuri katika michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge inayoendelea nchini Ethiopia.
Kili
Stars jana imekata tiketi ya Robo Fainali, baada ya kuichapa Rwanda
mabao 2-1 katika mchezo wa Kundi A na kufikisha pointi sita baada ya
mechi mbili, kutokana na awali kuifunga Somalia 4-0.
Na
sasa timu hiyo ya Kocha Alhaj Abdallah Athumani Seif ‘King Kibaden’
itaingia kwenye mchezo wa mwisho dhidi ya wenyeji, Ethiopia kutafuta
kuendelea kuongoza kundi hilo.
“Tunamshukuru
Mungu kwa matokeo haya, lakini hapa bado sana, tunajua tuna deni kubwa
kwa Watanzania ambao wana kiu ya kufurahia mafanikio ya timu
yao,”amesema Bocco.
Mshambuliaji huyo wa Azam FC amesema kwamba wataendelea kujitahidi katika mechi zijazo waendelee kushinda hadi kutwaa ubingwa.
“Tunajua
Watanzania wamekata tamaa na timu yao, hususan kutokana na mwenendo
mbaya katika siku za karibuni. Hilo ni deni letu sisi wachezaji na
tutajitahidi tuwafariji,”amesema Bocco.
Michuano
ya CECAFA Challenge inaendelea leo kwa michezo minne ya makundi yote,
Kenya dhidi ya Burundi Kundi B, Somalia dhidi ya Ethiopia Kundi A na ya
Kundi C, kati ya Malawi na Djibouti na Sudan Kusini dhidi ya Sudan.
Kesho
ni mapumziko na keshokutwa mechi za makundi zitahitimishwa kwa michezo
mine pia, Rwanda dhidi ya Somalia, Kili Stars na Ethiopia Kundi A,
Zanzibar na Kenya, Uganda na Burundi Kundi B, Sudan Kusini na Malawi,
Djibouti na Sudan Kundi C.
Hakuna maoni :