SIASA

SIASA

MAONI

MAONI

BURUDANI

MICHEZO

/ / PLUIJM: HII RATIBA YA LIGI KUU BARA INANIVURUGA KUPITA KIASI

Kocha Mkuu wa Yanga, Mholanzi, Hans van Der Pluijm, ameweka wazi kuwa, ratiba ya ligi imekuwa ni kikwazo kwake cha kuandaa program za muda mrefu.


Kwa sasa Yanga inaendelea na mazoezi yake ikiwa na wachezaji wachache wa kikosi cha kwanza kutokana na wengi wao kuwepo katika timu zao za taifa kwa ajili ya michuano ya Chalenji inayofanyika mjini Addis Ababa, Ethiopia.  

Pluijm alisema kuwa anaweza kusema kuwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limekuwa likipanga ratiba ya ligi vibaya ambapo huwa inavuruga utaratibu mzima wa uboreshaji wa timu.

“Nashangaa TFF sijui wanapangaje ratiba yao, ligi inasimamasimama bila mpangilio, wachezaji wanatumika sana nje ya klabu zao, hii ipo tofauti kabisa na nchi nyingine ulimwenguni.

“Ratiba hii inaharibu kabisa programu zangu kwani kwa kipindi kirefu huwa nawakosa wachezaji wangu muhimu, hivyo siwezi kuwapa mbinu za kupambana katika ligi ili tuweze kuwa mabingwa mwishoni mwa msimu.


“Kama kipindi hiki ligi imekolea lakini tumelazimika kusimama ili wachezaji wetu waende kujiunga na timu ya taifa kwa ajili ya mechi za kufuzu Kombe la Dunia, mechi zimeisha wanaenda Ethiopia kwa ajili ya Michuano ya Chalenji, hapa sitaweza kabisa kukipa mazoezi kamili kikosi changu chote kwa kuwa wengi wao wa kikosi cha kwanza hawapo,” alisema Pluijm.


«
Next

Chapisho Jipya

»
Previous

Taarifa za zamani

About Unknown

Asante kwa kutembelea SELASINI HABARI,NITAKUHABARISHA, KUKUELIMISHA NA KUKUBURUDISHA HIVYO USIKOSE KUTEMBELEA SELASINIHABARI.BLOGSPOT.COM.

Hakuna maoni :

Leave a Reply