SIASA

SIASA

MAONI

MAONI

BURUDANI

MICHEZO

/ / UEFA CHAMPIONZ LIGI-JUMATANO MAN UNITED-PSV: TATHMINI, HALI ZA VIKOSI!


MANUNITED-PSVWAKIWA kileleni mwa Kundi B la UEFA CHAMPIONZ LIGI, UCL, Manchester United wanahitaji ushindi kwenye Mechi yao hii na PSV Eindhoven Uwanjani Old Trafford ili wafuzu kutinga Raundi ya Mtoano ya Timu 16 huku wakiwa na Mechi moja mkononi.

Lakini PSV, inayoongozwa na Kocha Phillip Cocu, ambae alikuwa Mchezaji chini ya Meneja wa Man United Louis van Gaal huko Barcelona, iliifunga Man United 2-1 katika Mechi ya kwanza huko Amsterdam.

Kuelekea Mechi hii:
Man United wanatinga kwenye Mechi hii wakiwa na morali baada ya kulishinda lile wimbi la Droo 3 za 0-0 Mwezi Oktoba na kufanikiwa kupachika Mabao katika Mechi zao 3 zilizopita huku Wachezaji wao Watano tofauti wakifunga katika Mechi hizo wakizibwaga CSKA Moscow 1-0, WBA 2-0 na Watford 2-1.

Katika Mechi yao ya mwisho Majuzi Jumamosi Man United waliyoifunga Watford kwenye Ligi Kuu England na kupanda hadi Nafasi ya Pili, mmoja wa Wafungaji wao alikuwa Memphis Depay ambaye pia ndie aliefungana Bao la Man United walipocheza na Timu yake ya zamani PSV.

PSV wanaingia Mechi hii ya Old Trafford wakiwa hawajashinda hata Mechi moja ya Kundi B la UCL ya Ugenini baada ya kufungwa na CSKA Moscow na Wolfsburg.

Kwenye Ligi yao huko Uholanzi, PSV wako Nafasi ya Pili baada ya Juzi Jumamosi kuongoza 1-0 walipocheza na Willem II na kutoka Sare 2-2.

Hali za Wachezaji:
Louis van Gaal Leo amepata afueni baada ya Kepteni wake Wayne Rooney, Anthony Martial na Marouane Fellaini wote kurejea mazoezini na wote kuwa fiti kwa ajili ya Mechi hii baada ya kuikosa Mechi ya Jumamosi na Watford.

Wachezaji wenye maumivu na kuwa na hatihati ni Bastian Schweinsteiger, Phil Jones, James Wilson na Ander Herrera wakati Majeruhi ni Michael Carrick, Valencia na Luke Shaw ambae alivunjwa Mguu mara mbili kwenye Mechi ya kwanza na PSV.

Kwa upande wa PSV, Hector Moreno, ambae ndie alimvunja Mguu Luke Shaw, yupo kwenye maumivu na huenda asiwepo pamoja na Maxime Lestienne na Simon Poulsen.

Kumbukumbu:
Man United ishacheza na PSV mara 5 tangu wakutane kwa mara ya kwanza 1984 walipokutana kwenye UEFA CUP na Man United kushinda 1-0 Uwanjani Old Trafford na kuibwaga PSV Jumla ya Bao 1-0 kwa Mechi 2 na kisha kucheza kwenye Kundi la UCL Msimu wa 2000/01 ambapo PSV wlishinda 3-1 kwao lakini Old Trafford Man United iliitwanga PSV Bao 3 kwa Bao za Teddy Sheringham, Paul Scholes na Dwight Yorke.

Hivyo katika mara mbili walizocheza Old Trafford Man United walishinda Mechi zote 2.



Mtu hatari:
Kwa PSV ni Luuk de Jong ambae ndie anaoongoza kufunga Mabao kwa Timu yake na pia Ligi ya Uholanzi, Eredivisie, Msimu huu akiwa na Bao 11 lakini kwenye UCL Msimu huu amefunga Bao 1 dhidi ya Wolfsburg.

VIKOSI VINATARAJIWA KUWA:
Man United: David de Gea, Matteo Darmian, Marcos Rojo, Chris Smalling, Daley Blind, Jesse Lingard, Juan Mata, Morgan Schneiderlin, Bastian Schweinsteiger, Ashley Young, Memphis Depay
PSV Eindhoven: Jeroen Zoet, Santiago Arias, Joshua Brenet, Jeffrey Bruma, Héctor Moreno, Andrés Guardado, Adam Maher, Davy Pröpper, Luuk de Jong, Jürgen Locadia, Luciano Narsingh
REFA: Pavel Kralovec [Czech Republic]
UCL-GRPB-NOV24
UEFA CHAMPIONZ LIGI
RATIBA
**Mechi zote kuanza Saa 4 Dak 45 Usiku, isipokuwa inapotajwa
Jumanne Novemba 24
KUNDI E
2000 BATE Borislov v Bayer Leverkusen           
Barcelona v AS Roma                 
KUNDI F
Arsenal v Dinamo Zagreb           
Bayern Munich v Olympiakos                
KUNDI G
FC Porto v Dynamo Kiev             
Maccabi Tel Aviv v Chelsea          
KUNDI H
2000 Zenit Saint Petersburg v Valencia           
Lyon v KAA Gent              
Jumatano Novemba 25
KUNDI A
Malmö FF v Paris St Germaine              
Shakhtar Donetsk v Real Madrid           
KUNDI B
2000 CSKA v VfL Wolfsburg        
Man United v PSV Eindhoven               
KUNDI C
1800 FC Astana v Benfica           
Atletico Madrid v Galatasaray               
KUNDI D
Borussia Mönchengladbach v Sevilla                
Juventus v Man City 
       
UEFA CHAMPIONZ LIGI
Mechi za Mwisho za Makundi
RATIBA
**Mechi zote kuanza Saa 4 Dak 45 Usiku, isipokuwa inapotajwa
Jumanne Desemba 8
KUNDI A
Paris St Germain v Shakhtar Donetsk              
Real Madrid v Malmö FF             
KUNDI B
PSV v CSKA           
VfL Wolfsburg v Man United                 
KUNDI C
Benfica v Atletico Madrid            
Galatasaray v FC Astana             
KUNDI D
Man City v Borussia Mönchengladbach            
Sevilla v Juventus             
Jumatano Desemba 9
KUNDI E
Bayer Leverkusen v Barcelona               
Roma v BATE Borislov                
KUNDI F
Dinamo Zagreb v Bayern Munich           
Olympiakos v Arsenal                 
KUNDI G
Chelsea v FC Porto           
Dynamo Kiev v Maccabi Tel Aviv            
KUNDI H
KAA Gent v Zenit Saint Petersburg                 
Valencia v Lyon                

TAREHE MUHIMU:
-Ratiba Mechi za Makundi: 
Mechidei 1: 15/16 Septemba
Mechidei 2: 29/30 Septemba 
Mechidei 3: 20/21 Oktoba
Mechidei 4: 3/4 Novemba 
Mechidei 5: 24/25 Novemba 
Mechidei 6: 8/9 Decemba
Raundi za Mtoano:
-Droo ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16: Desemba 14
**Mechi Februari 16/17/23/24 na Marudiano Machi 8/9/15/16
-Droo ya Robo Fainali: Machi 18
**Mechi Aprili 5/6 na Marudiano Aprili 12/13
-Droo ya Nusu Fainali: Aprili 15
**Mechi Aprili 26/27 na Marudiano Mei 3/4
FAINALI
Mei 28
San Siro, Milan, Italy

«
Next

Chapisho Jipya

»
Previous

Taarifa za zamani

About Unknown

Asante kwa kutembelea SELASINI HABARI,NITAKUHABARISHA, KUKUELIMISHA NA KUKUBURUDISHA HIVYO USIKOSE KUTEMBELEA SELASINIHABARI.BLOGSPOT.COM.

Hakuna maoni :

Leave a Reply