Beki wa
pembeni wa Simba, Hassani Kessy, amefunguka na kutaja sababu inayomzuia asiongeze
mkataba ni timu hiyo kutoshiriki michuano ya kimataifa Afrika.
Kufikia
mwezi ujao, Kessy atakuwa amebakiza miezi sita katika mkataba wake na kwa
mujibu wa kanuni za Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa), anaruhusiwa kufanya
mazungumzo na klabu nyingine inayomhitaji ikiwemo Yanga ambayo inatajwa
kumuwania kwa ukaribu.
Yanga
itashiriki katika Ligi ya Mabingwa Afrika kutokana na kutwaa ubingwa wa Ligi
Kuu Bara msimu uliopita.
Kessy
amesema mipango aliyojiwekea ni kucheza soka la kimataifa nje ya Tanzania na
ndiyo maana amekuwa akisita kusaini mkataba mpya Simba.
“Sifikirii
kuongeza mkataba wa kubaki kuendelea kuichezea Simba katika kipindi kingine,
licha ya viongozi kuhitaji huduma yangu.
Hakuna maoni :