SIASA

SIASA

MAONI

MAONI

BURUDANI

MICHEZO

/ / Haya Hapa Majina 43 ya Wamiliki wa Makontena 329 Ambayo Yalipitishwa Bandarini Bila Kulipiwa Ushuru



Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA) juzi  ilitaja majina ya kampuni 43 na wamiliki wa makontena 329 ambayo yalipitishwa bandarini bila kulipiwa ushuru, na kufichuliwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa wiki iliyopita.

Akizungumza na waandishi wa habari juzi jijini Dar es Salaam, Kaimu Kamishna Mkuu wa TRA, Dk. Philip Mpango alisema Mamlaka hiyo iliagizwa na Waziri Mkuu Majaliwa kuchukua hatua mara moja kwa kufuatilia na kubaini wamiliki wa Bandari Kavu (ICD) zilizohusika katika kashfa hiyo.

Alisema mbali na hilo walitakiwa kuwatambua wamiliki wa makontena hayo, bidhaa zilizokuwemo, kuwalipisha wahusika kodi iliyokwepwa pamoja na kuwachukulia hatua watumishi waliohusika na upotevu huo.

Dk. Mpango aliyataja majina ya makampuni na watu binafsi na idadi ya makontena waliyopitisha bila kulipia ushuru (katika mabado) kuwa ni:-
Lotai Steel Tanzania Ltd (100)
Tuff Tryes Centre Company Ltd (58)
Binslum Tyres Company Ltd (33)
Tifo Global Mart Tanzania Company Limited (30)
IPS Roofing Company Limited (20)
Rushywheel Tyre Centre Co Ltd (12)
Kiungani Trading Co Ltd (10)
Homing International Limited (9)
Red East Building Materials Company Ltd (7)
Tybat Trading Co Limited (5)
Zing Ent Ltd (4)
Juma Kassem Abdul (3)
Salum Link Tyres (3)
Ally Masoud Dama (2)
CLA Tokyo Limited (2)
Farid Abdullah Salem (2)
Salum Continental Co Ltd (2)
Zuleha Abbas Ali (2)
Issa Ali Salim (2)
Snow Leopard Building (2)
Abdulaziz Mohamed Ally
Ahmed Saleh Tawred
Ali Amer
Ally Alhamdany
Awadhi Salim Saleh
Faheed Abdallah Said
Hani Said
Hassan Hussein Suleyman
Hamud Suleiman Enterprise
Kamil Hussein Ali
Libas Fashion
Nassir Salehe Mazrui
Ngiloi Ulomi Enterprises Co Ltd
Omar Hussein Badaway
Said Ahmad Hamdan
Said Ahmed Said
Salumu Peculiar Tyres
Sapato N. Kyando
Simbo Yonah Kimaro
Strauss International Co. Ltd
Swaleh Mohamed Swaleh
Alisema kwa ujumla, makampuni hayo yalipitisha makontena 329 ambayo yaliondolewa kinyume cha taratibu kutoka ICD ya Azam inayomilikiwa na Said Salim Bakhresa And Company Limited.

Dk. Mpango alisema bidhaa zilizokuwemo ndani ya makontena hayo ni pamoja na matairi ya magari, samani mbalimbali, betri za magari, vifaa vya ujenzi, nguo na bidhaa zingine mchanganyiko.

«
Next

Chapisho Jipya

»
Previous

Taarifa za zamani

About Unknown

Asante kwa kutembelea SELASINI HABARI,NITAKUHABARISHA, KUKUELIMISHA NA KUKUBURUDISHA HIVYO USIKOSE KUTEMBELEA SELASINIHABARI.BLOGSPOT.COM.

Hakuna maoni :

Leave a Reply