SIASA

SIASA

MAONI

MAONI

BURUDANI

MICHEZO

/ / SAMATTA, ULIMWENGU MGUU SAWA JAPAN, TAYARI WAIJUA TIMU WATAKAYOANZA NAYO KOMBE LA DUNIA



Mabingwa wa Afrika, TP Mazembe sasa wamejua mpinzani wao wa kwanza katika michuano ya Kombe la Dunia kwa klabu.

Mazembe inakutana na Sanfrecce Hiroshima ya Japan ambayo leo imeanza michuano hiyo vizuri kwa kuichapa Auckland City ya New Zealand.

Mabao mawili ya Minagawa na Shotani, yalitosha kuwapa ushindi wenyeji hao na sasa wanakutana na TP Mazembe Jumapili.

Watanzania Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wanatarajia kuongoza mashabulizi ya Mazembe ambayo tayari ipo mjini Osaka kwa ajili ya mechi ya Jumapili.

Kiutaratibu wa michuano hiyo, TP Mazembe imepewa nafasi ya kuanzia robo fainali, ikishinda mechi ya Jumapili, itacheza nusu fainali desemba 16 dhidi ya River Plate ya Argentina, ikishinda, basi ndiyo fainali.

«
Next

Chapisho Jipya

»
Previous

Taarifa za zamani

About Unknown

Asante kwa kutembelea SELASINI HABARI,NITAKUHABARISHA, KUKUELIMISHA NA KUKUBURUDISHA HIVYO USIKOSE KUTEMBELEA SELASINIHABARI.BLOGSPOT.COM.

Hakuna maoni :

Leave a Reply