SIASA

SIASA

MAONI

MAONI

BURUDANI

MICHEZO

/ / KEPTENI ROONEY AIPELEKA MAN UNITED RAUNDI YA 4 FA CUP.


MANUNITED-ROONEY-PENATI-GOLIBAO la Penati ya Dakika ya 93 iliyofungwa na Kepteni Wayne Rooney imewaingiza Manchester United Raundi ya 4 ya FA CUP walipoitungua Timu ya Daraja la chini Sheffield United 1-0 Uwanjani Old Trafford.

Penati hiyo ilitolewa katika Dakika ya 92 baada ya Memphis Depay, alieingizwa Kipindi cha Pili na kuleta uhai mkubwa kwenye mashambulizi, kumtambuka John Brayford na kuingia ndani ya Boksi na kuchezewa Rafu na Dean Hammond.

Bao hilo la Rooney lilileta ahueni kubwa kwa Man United kwani walitawala Mechi yote, kwa Asilimia 72 lakini walilenga Shuti 1 tu Golini dhidi ya Timu ya Daraja la chini ambayo iliamua kujihami.

Man United watajua wapinzani wanaofuatia baada ya Droo ya Raundi ya 4 ambayo itafanyika Jumatatu Usiku.

VIKOSI:
Manchester United: David de Gea, Darmian, Smalling, Blind, Borthwick-Jackson, Fellaini, Schweinsteiger, Mata, Herrera, Martial, Rooney
Akiba: Depay, Romero, Varela, McNair, Lingard, Pereira, Keane
Sheffield United: Long, Brayford, Edgar, Collins, McEveley, Coutts, Basham, Hammond, Woolford, Sammon, Sharp
Akiba: Howard, Flynn, Baxter, Done, Campbell-Ryce, Reed, Adams
REFA: Andre Marriner
FA CUP
Raundi ya 3
***Saa za Bongo
Ijumaa Januari 8
Exeter 2 Liverpool 2
Jumamosi Januari 9
Wycombe 1 Aston Villa 1  
Arsenal 3 Sunderland 1              
Birmingham 1 Bournemouth 2              
Brentford 0 Walsall 1        
Bury 0 Bradford 0            
Colchester 2 Charlton 1              
Doncaster 1 Stoke 2         
Eastleigh 1 Bolton 1         
Everton 2 Dag & Red 0              
Hartlepool 1 Derby 2                  
Huddersfield 2 Reading 2           
Hull 1 Brighton 0              
Ipswich 2 Portsmouth 2             
Leeds 2 Rotherham 0                 
Middlesbrough 1 Burnley 2         
Newport v Blackburn [IMEAHIRISHWA]           
Northampton 2 MK Dons 2         
Norwich 0 Man City 3                 
Nottm Forest 1 QPR 0
Peterborough 2 Preston 0           
Sheff Wednesday 2 Fulham 1               
Southampton 1 Crystal Palace 2            
Watford 1 Newcastle 0               
West Brom 2 Bristol City 2          
West Ham 1 Wolves 0      
Man United 1 Sheffield United 0            
Jumapili Januari 10
1500 Oxford United v Swansea             
1700 Carlisle v Yeovil                 
1700 Chelsea v Scunthorpe                  
1900 Tottenham v Leicester                 
2100 Cardiff v Shrewsbury          
 

THE EMIRATES FA CUP 2015/16
TAREHE MUHIMU
Raundi ya 3
Ijumaa 9 Januari 2016
Raundi ya 4
Jumamosi 30 Januari 2016
Raundi ya 5
Jumamosi 20 Februari 2016
Raundi ya 6-Robo Fainali
Jumamosi 12 Machi 2016
Nusu Fainali
Jumamosi 23 Aprili 2016 & Jumapili 24 Aprili 2016
Fainali
Jumamosi 21 Mei 2016

«
Next

Chapisho Jipya

»
Previous

Taarifa za zamani

About Unknown

Asante kwa kutembelea SELASINI HABARI,NITAKUHABARISHA, KUKUELIMISHA NA KUKUBURUDISHA HIVYO USIKOSE KUTEMBELEA SELASINIHABARI.BLOGSPOT.COM.

Hakuna maoni :

Leave a Reply