SIASA

SIASA

MAONI

MAONI

BURUDANI

MICHEZO

/ / KEPTENI ROONEY NDIE MCHEZAJI BORA ENGLAND 2015, AZOA TUZO MARA YA PILI MFULULIZO!

ROONEY-ENGLANDKEPTENI wa Manchester United, Wayne Rooney, ametwaa Tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwaka kwa 2015 akitetea tena Tuzo ambayo pia aliizoa 2014.
 
Hii ni mara ya 4 kwa Rooney kuzoa Tuzo hii ambayo Wachaguaji wake ni Masapota wa Timu ya Taifa ya England.
 
Mapema Desemba England ilianika Listi ya Wagombea wa Tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwaka kwa Nchi yao ambapo pia ipo Tuzo kwa Chipukizi Vijana wa chini wa Miaka 21, U-21.
 
Kepteni wa England, Wayne Rooney, ambae alishinda Tuzo hiyo Mwaka Jana, ni miongoni mwa Wachezaji Watano waliokuwa wakiigombea.
 
Rooney Mwaka 2015 aliiongoza England kufuzu kuingia Fainali za Mataifa ya Ulaya, EURO 2016, ambazo zitachezwa huko France Mwezi Juni huku akihakikisha England inashinda Mechi zao zote 10 za Kundi lao na kuifungia Jumla ya Bao 5 kwa Mwaka 2015 kwa England huku pia akiivunja Rekodi ya Sir Bobby Charlton ya Ufungaji Bora katika Historia ya England kwa kufunga Bao 50 Rekodi ambayo iliwekwa na Charlton Mwaka 1968 alipofunga Bao lake la 49.
 
++++++++++++++++++++++++++++++++++
Wagombea Tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwaka:
Joe Hart (Manchester City)
Gary Cahill (Chelsea)
Raheem Sterling (Manchester City)
Wayne Rooney (Manchester United)
Harry Kane (Tottenham Hotspur)
++++++++++++++++++++++++++++++++++
Kwa Vijana wa U-21, Listi ya Wagombea Watano nayo ilianikwa.
++++++++++++++++++++++++++++++++++
Wagombea Tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwaka kwa U-21:
Jack Butland (Stoke City)
Carl Jenkinson (West Ham United)
James Ward-Prowse (Southampton)
Jesse Lingard (Manchester United)
Nathan Redmond (Norwich City)
++++++++++++++++++++++++++++++++++
Kura kwa Wagombea hawa zilipigwa Mtandaoni na Masapota wa England na upigaji ulifungwa Jumapili Januari 3.
Rooney alijizolea Kura Asilimia 37, Harry Kane 30% na Hart 19%.
Kwa upande wa Vijana U-21 Kipa wa Stoke Jack Butland ndie Mshindi.

«
Next

Chapisho Jipya

»
Previous

Taarifa za zamani

About Unknown

Asante kwa kutembelea SELASINI HABARI,NITAKUHABARISHA, KUKUELIMISHA NA KUKUBURUDISHA HIVYO USIKOSE KUTEMBELEA SELASINIHABARI.BLOGSPOT.COM.

Hakuna maoni :

Leave a Reply