SIASA

SIASA

MAONI

MAONI

BURUDANI

MICHEZO

/ / TFF Wakiri Kulikoroga Suala la Azam Kupewa Ruhusa Kwenda Zambia..Malinzi Aomba Radhi.

Rais wa TFF Bw. Jamal Malinzi ameviomba radhi vilabu vya ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara kutokana na timu ya Azam kupewa ruhusa na TFF kwenda nchini Zambia kushiriki mechi za kirafiki ambazo hazipo kwenye kalenda ya CAF, FIFA wala chama chochote cha soka kati ya Tanzania na Zambia.

Malinzi amekiri makosa yamefanyika ndani ya TFF kuiruhusu Azam lakini amejitetea kwamba wakati ruhusa hiyo inatolewa yeye hakuwepo nchini.
Malinzi pia amesema Yanga kutofanya uchaguzi mkuu wa viongozi wa klabu yao haimaanishi kwamba wako juu ya sheria na amewataka Yanga kuheshimu katiba yao pamoja na ile ya TFF.

“Naomba nivitake radhi vilabu vyote 15 vinavyoshirili ligi kuu Tanzania bara kwa kosa lililofanyika la kuwaruhusu Azam FC kwenda Zambia kucheza mechi za kirafiki, najua maamuzi yamefanyika mimi nikiwa Burundi, lakini kama kiongozi nakiri kosa kufanyika na naviomba radhi vilabu vyote”.

“Kuhusu Yanga kutofanya uchaguzi ukweli ni kwamba, Yanga hawapo juu ya sheria na wanapaswa kuheshimu katiba yao na ya TFF”.

Kuondoka kwa Azam kunasababisha mechi zinazoihusu timu hiyo kusogezwa mbele na kusababisha viporo vya mechi visivyokuwa vya lazima na kuvisababishi gharama na usumbufu vilabu ambavyo vingecheza na Azam mechi hizo.

Malinzi pia ametuma salu za rambirambi kwa familia, ndugu jamaa na marafiki wa  Epaphra Swa aliyefariki jana asubuhi kwenye hospitali ya Muhimbili jijini Dar es Salaam.

Epaphra Swai alikuwa ni Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) na Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu mkoa wa Simiyu.

«
Next

Chapisho Jipya

»
Previous

Taarifa za zamani

About Unknown

Asante kwa kutembelea SELASINI HABARI,NITAKUHABARISHA, KUKUELIMISHA NA KUKUBURUDISHA HIVYO USIKOSE KUTEMBELEA SELASINIHABARI.BLOGSPOT.COM.

Hakuna maoni :

Leave a Reply