SIASA

SIASA

MAONI

MAONI

BURUDANI

MICHEZO

/ / WENGER – ‘DIEGO COSTA AMETUGHARIMU KWA MARA NYINGINE TENA.


ARSENAL-CHELSEA-REDCARDMENEJA wa Arsenal Arsene Wenger amesema Timu yao kwa mara nyingine tena wamekuwa waathirika wa Straika wa Chelsea Diego Costa aliesababisha Senthafu wao Per Mertesacker adungwe Kadi Nyekundu katika Dakika ya 18 kwenye Mechi iliyochezwa Jumapili huko Emirates na Chelsea kuifunga Arsenal 1-0.
 
Dakika 5 baada ya Mertesacker kutolewa nje, Diego Costa alifunga Bao pekee na la ushindi kwa Chelsea.
 
Wenger ameeleza: “Costa amesababisha Wachezaji wetu Wawili wapewe Kadi Nyekundu katika Mechi zetu 2 zilizopita. Je ni uamuzi sahihi au hapana? Sijui. Huo ni ukweli bila kumtuhumu chochote!”
 
Mwezi Septemba Mwaka Jana, Costa alikwaruzana na Sentahafu wa Arsenal Gabriel ambae alitolewa nje kwa Kadi Nyekundu kwa tukio hilo na Chelsea kuibuka kidedea kwa kuifunga Arsenal 2-0.
 
Msimu huu, Arsenal wamezoa Kadi Nyekundu 3 na zote ni za kwenye Mechi dhidi ya Chelsea baada ya pia Santi Cazorla kutolewa nje katika Mechi hiyo hiyo aliyotolewa Gabriel huko Stamford Bridge.
 
Arsenal wamezoa Kadi Nyekundu 7 kwenye Mechi na Chelsea na hizo ni nyingi kupitana kwenye mapambano yao na Timu nyingine yeyote kwenye Ligi Kuu England.
 
Akielezea tukio la Jana la Mertesacker kumwangusha Costa akiwa Mtu wa mwisho huku Costa akielekea Golini, Wenger amesema hajui kama Costa alikuwa Ofsaidi au Mertesacker alimgusa na kumwangusha Costa.
 
Wenger amesema: “Refa alikuwa mwepesi kutoa Kadi Nyekundu. Lakini tulilikabili tukio hilo vizuri na tulistahili Sare.”
Alipohojiwa kama Costa alitengeneza tukio hilo, Wenger alijibu: “Ndio. Hiyo ndio Gemu ya Straika. Diego Costa ni mzuri kwa hayo!”
 
Lakini Bosi wa Chelsea, Guus Hiddink, hakukubaliana na amesema: "Kulikuwa hamna wasiwasi. Ni pasi safi na Costa angeweza kwenda moja kwa moja kumkabili Kipa Petr Cech lakini aliangushwa. Hilo ni wazi!”

«
Next

Chapisho Jipya

»
Previous

Taarifa za zamani

About Unknown

Asante kwa kutembelea SELASINI HABARI,NITAKUHABARISHA, KUKUELIMISHA NA KUKUBURUDISHA HIVYO USIKOSE KUTEMBELEA SELASINIHABARI.BLOGSPOT.COM.

Hakuna maoni :

Leave a Reply