SIASA

SIASA

MAONI

MAONI

BURUDANI

MICHEZO

/ / BEKI SIMBA AJIONDOA KIKOSINI, SIKU NNE TU KABLA YA KUIVAA YANGA.


Beki wa Simba, Abdi Banda jana, amejiondoa katika kikosi cha Simba kinachotarajia kuivaa Yanga kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Banda amesema ameumia na atakaa nje ya uwanja kwa miezi miwili huku akijipa matumaini, lakini Simba wakaonekana kutotaka kulizungumzia suala hilo.

Banda ambaye ana uwezo wa kucheza hadi namba nne tofauti uwanjani, alithibitisha kupata majeraha yake ya misuli kupitia Ukurasa wa Kijamii wa Facebook aliyeandika ujumbe uliosomeka hivi: “Dah nitamis sana kurudi uwanjani, miezi miwili ni mingi sana, dah ila ntapona.”


Ujumbe wa beki huyo, uliendana na picha yake aliyoiweka akiwa amelala kitandani hospitalini akifanyiwa vipimo.


Daktari wa Simba wala viongozi, hakuna aliyekuwa tayari kulizungumzia suala hilo, kwani baada ya muda fulani, Banda alifuta ile post yake kwenye Facebook.

«
Next

Chapisho Jipya

»
Previous

Taarifa za zamani

About Unknown

Asante kwa kutembelea SELASINI HABARI,NITAKUHABARISHA, KUKUELIMISHA NA KUKUBURUDISHA HIVYO USIKOSE KUTEMBELEA SELASINIHABARI.BLOGSPOT.COM.

Hakuna maoni :

Leave a Reply