SIASA

SIASA

MAONI

MAONI

BURUDANI

MICHEZO

/ / COPA DEL REY: BARCA SARE, WATINGA FAINALI.

3539MABINGWA Watetezi wa Kombe la Mfalme wa Spain ambalo huitwa Copa del Rey, FC Barcelona, Jana walitoka Sare 1-1 na Valencia katika Mechi ya Pili ya Nusu Fainali na kutinga Fainali kwa Jumla ya Mabao 8-1.
Katika Mechi ya kwanza Barca walinyuka Valencia 8-0.
 
Jana huko Mestalla, Valencia, walio chini ya Garry Neville, Mchezaji wa zamani wa Manchester United, walitangulia kufunga kwa Bao la Alvaro Negredo lakini Barca, wakicheza bila ya Mastaa wao wengi walisawazisha kwa Bao la Wilfrid Kaptoum alietokea Benchi.
 
Kwenye Fainali, Barca watacheza na Mshindi kati ya Celta Vigo na Sevilla ambao wanarudiana Leo huku Sevilla wakiwa wameshinda 4-0 katika Mechi ya kwanza.
VIKOSI VILIVYOANZA:
Valencia
Domenech; Vezo, Santos, Diallo, Gaya; Danilo, Villalba, Zahibo; Mina, Negredo, Piatti
Barcelona:
Ter Stegen; Adriano, Bartra, Vermaelen, Mathieu; Rakitic, Samper, Sergi; Vidal, Munir, Sandro

«
Next

Chapisho Jipya

»
Previous

Taarifa za zamani

About Unknown

Asante kwa kutembelea SELASINI HABARI,NITAKUHABARISHA, KUKUELIMISHA NA KUKUBURUDISHA HIVYO USIKOSE KUTEMBELEA SELASINIHABARI.BLOGSPOT.COM.

Hakuna maoni :

Leave a Reply