SIASA

SIASA

MAONI

MAONI

BURUDANI

MICHEZO

/ / PAMOJA NA KUSHINDA, MASHABIKI WA YANGA WAONGOZA KWA KUZIMIA UWANJA WA TAIFA.


Pamoja na ushindi wa bao 2-0 dhidi ya Simba kuonekana ni mtamu kwa mashabiki wa Yanga, wao ndiyo waliongoza kwa kuzimia.

Mashabiki 18 walizimia kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam na kutibiwa hiyo jana huku wa Simba wakiwa ni nane tu.

Mmoja wa wahudumu wa Vijana wa Skauti alisema mashabiki waliokuwa na jezi za rangi ya njano ndiyo walikuwa wengi zaid.

“Wengine tuliwapatia huduma palepale walipokuwa, lakini wengine tulisaidiana na watu wa huduma ya kwanza na kuwapeleka ndani,” alisema lakini akasisitiza yeye si msemaji.

Katika mechi hiyo mashabiki wengi wa Simba walijitokeza huku wakionyesha kuiamini zaidi timu yao iliyokuwa imecheza mechi sita za ligi bila ya kupoteza hata moja.


Lakini bao moja katika kila kipindi baada ya beki wake Abdi Banda kuwa amelambwa kadi nyekundu, lilifanya waone kama hawaamini kilichokuwa kikitokea huku wa Yanga waliokuwa na hofu ya kipigo, walionekana kuzidiwa na furaha.

«
Next

Chapisho Jipya

»
Previous

Taarifa za zamani

About Unknown

Asante kwa kutembelea SELASINI HABARI,NITAKUHABARISHA, KUKUELIMISHA NA KUKUBURUDISHA HIVYO USIKOSE KUTEMBELEA SELASINIHABARI.BLOGSPOT.COM.

Hakuna maoni :

Leave a Reply