SIASA

SIASA

MAONI

MAONI

BURUDANI

MICHEZO

/ / TAMBWE AANZA KUISOMA NAMBA YA HAMISI KIIZA, AMTIMULIA VUMBI KWA MABAO.



Mganda Hamisi Kiiza ameonyesha kweli amepania kufanya vema zaidi na kupachika mabao kila inapowezekana kuisaidia Simba.

Kiiza amefunga mabao mawili leo na kuisaidia Simba kushinda kwa 2-1 dhidi ya Stand United, sasa ndiyo vinara wa Ligi kuu Tanzania Bara baada ya kufikisha pointi 44.

Mabao hayo mawili, yamekuwa msaada kwa Simba lakini msaada kwa Kiiza ambaye amefikisha mabao 16 na kumpita mshindani wake mkuu katika upachikaji mabao, Amissi Kiiza wa Yanga mwenye 14.

Kiiza alikuwa akiitumikia Yanga nchini Mauritius katika mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika. Kuna nafasi ya kufunga katika mechi ijayo lakini tayari Kiiza aliyekuwa nyuma yake kwa mabao manne, sasa amempita.

Donald Ngoma ana mabao 10 sawa na Jeremiah wa Prisons na Elius Maguri wa Stand United ana 9 akiwa amekwama hapo muda mrefu sasa.

«
Next

Chapisho Jipya

»
Previous

Taarifa za zamani

About Unknown

Asante kwa kutembelea SELASINI HABARI,NITAKUHABARISHA, KUKUELIMISHA NA KUKUBURUDISHA HIVYO USIKOSE KUTEMBELEA SELASINIHABARI.BLOGSPOT.COM.

Hakuna maoni :

Leave a Reply