SIASA

SIASA

MAONI

MAONI

BURUDANI

MICHEZO

/ / VPL: JUMATANO AZAM V STAND, IJUMAA TWIGA KUPAA HARARE


VPL-SIT-LOGOLigi Kuu ya Vodacom Tanzania (VPL) inatarajiwa kuendelea kesho Jumatano kwa mchezo mmoja, ambapo Azam FC watawakaribisha Stand United katika uwanja wa Azam Complex Chamazi.
 
Ijumaa mkoani Shinyanga katika uwanja wa Kambarage, wakata miwa wa Kagera Sugar watakua wenyeji wa ndugu zao kutoka wakata miwa Mtibwa Sugar kutoka Manungu Turiani.
 
Wikiendi Jumamosi na Jumapili ligi hiyo itaendelea kwa michezo mitano kuchezwa katikwa viwanja mbalimbali nchini, jijini Tanga wenyeji Coastal Union wakiwa wenyeji wa Simba SC katika uwanja wa Mkwakwani jijini humo.
 
Majimaji FC itakua nyumbani katika uwanja wa Majimaji mjini Songea kucheza na Mbeya City, huku chama la wana Stand United wakiwakaribisha Ndanda FC katika uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga.
 
Jumapili African Sports watakua wenyeji wa maafande wa jeshi la magereza Tanzania Prisons kwenye uwanja wa Mkwakwani jijii Tanga, huku siku ya Jumatatu Mgambo Shooting wakicheza dhidi ya Toto Africans jijini Tanga katika uwanja wa Mkwakwani.
 
TWIGA STARS KUWAFUATA ZIMBABWE IJUMAA
Timu ya Taifa ya Wanawake ya Mpira wa Miguu “Twiga Stars” inatarajiwa kusafiri siku ya Ijumaa kuelekea nchini Zimbabwe kwa ajili ya mchezo wake wa marudiano wa kuwania kufuzu kwa Fainali za Mataifa Afrika kwa Wanawake zitakazofanyika mwishoni mwa mwaka huu nchini Cameroon.
 
Kikosi cha Twiga Stars kinaendelea na mazoezi katika uwanja wa Karume chini ya kocha mkuu, Nasra Juma kujiandaa na mchezo huo muhimu ili kuweza kusonga mbele katika hatua inayofuata.
 
Kuhusu maendeleo ya kambi, kocha Nasra Juma amesema vijana wake wanaendela vizuri, wamekua wakiendelea na mazoezi tangu baada ya mchezo wa awali na ana imani watafanya vizuri katika mchezo wa marudiano.
 
Twiga Stars inahitaji ushindi katika mchezo huo wa marudiano utakaochezwa Jumapili, Machi 20 katika uwanja wa Rufalo uliopo jijini Harare ili kuweza kufuzu kwa hatua ya pili ya michuano hiyo.

«
Next

Chapisho Jipya

»
Previous

Taarifa za zamani

About Unknown

Asante kwa kutembelea SELASINI HABARI,NITAKUHABARISHA, KUKUELIMISHA NA KUKUBURUDISHA HIVYO USIKOSE KUTEMBELEA SELASINIHABARI.BLOGSPOT.COM.

Hakuna maoni :

Leave a Reply