SIASA

SIASA

MAONI

MAONI

BURUDANI

MICHEZO

/ / NGOMA: HATA SIKU YA SIMBA, BADO NITAFUNGA TU



Mshambuliaji wa Yanga, Donald Ngoma amesema mechi dhidi ya Simba, itakuwa kama mechi nyingine na ana uhakikaa atafunga.


Ngoma raia wa Zimbabwe, amefikisha mabao matatu katika mechi zake tatu za Ligi Kuu Bara. Mechi ya nne ni dhidi ya Simba, wikiendi ijayo.

"Nimeanza kuona ugumu wa ligi, lakini ninaona pia napata uzoefu na kujua cha kufanya. Simba ni watani wa Yanga lakini ni timu kama nyingine.

"Kufunga hakuwezi kuwa asilimia mia, lakini ninaamini uwezo wangu, ninawaamini wenzangu na ninaiamini timu kwa ujumla na ushirikiano wetu.

"Litakalotokea kama ni kufunga au kutoa pasi, lakini kikubwa Yanga ishinde ili twende na mwendo huu," alisema Ngoma.

«
Next

Chapisho Jipya

»
Previous

Taarifa za zamani

About Unknown

Asante kwa kutembelea SELASINI HABARI,NITAKUHABARISHA, KUKUELIMISHA NA KUKUBURUDISHA HIVYO USIKOSE KUTEMBELEA SELASINIHABARI.BLOGSPOT.COM.

Hakuna maoni :

Leave a Reply