DABI MANCHESTER, HAKUNA MBABE, SPURS YAFUMUA 5, HARRY KANE HETITRIKI!
LIGI KUU ENGLAND
RATIBA/MATOKEO:
Jumapili Oktoba 25
Sunderland 3 Newcastle 0
Bournemouth 1 Tottenham 5
Man United 0 Man City 0
1915 Liverpool v Southampton
Man City Leo wamerudi tena kileleni mwa Ligi Kuu England baada ya kutoka Sare ya 0-0 huko Old Trafford na Man United kwenye Dabi ya Jiji la Manchester.
Mechi hii ilikosa Mashuti yeyote yaliyolenga Magoli licha ya Man United kutawala kwa kipindi kirefu.
Shuti la kwanza kabisa Golini lilikuja mwishoni katika Dakika ya 82 wakati shuti la Jesus Navas kudakwa na Kipa wa Man United David De Gea na Dakika ya 84 Man United nusura wapate Bao baada ya mkwaju wa Jesse Lingard kugonga posti ya juu na kisha Kipa Joe Hart kuokoa shuti la Chris Smalling.
Katika Mechi nyingine ya Ligi Kuu England, Bournemouth wakiwa kwao walitandikwa Bao 5-1 na Tottenham huku Harry Kane akipiga Hetitriki.
Bao nyingine za Spurs zilifungwa na Mousa Dembele na Erik Lamela wakati Bao pekee la Bournemouth likifungwa na Matt Ritchie.
VIKOSI:
Manchester United: De Gea; Valencia, Jones, Smalling, Rojo; Schweinsteiger, Schneiderlin; Mata, Ander Herrera, Martial; Rooney
Akiba: Depay, Carrick, Blind, Romero, Fellaini, Lingard, Darmian.
Manchester City: Hart; Sagna, Kompany, Otamendi, Kolarov; Fernando, Fernandinho, De Bruyne, Toure, Sterling, Bony
Akiba: Zabaleta, Caballero, Jesus Navas, Mangala, Demichelis, Roberts, Iheanacho.
REFA: Mark Clattenburg
LIGI KUU ENGLAND
RATIBA:
**Saa za Bongo
Jumamosi Oktoba 31
1545 Chelsea v Liverpool
1800 Crystal Palace v Man United
1800 Man City v Norwich
1800 Newcastle v Stoke
1800 Swansea v Arsenal
1800 Watford v West Ham
1800 West Brom v Leicester
Jumapili Novemba 1
1630 Everton v Sunderland
1900 Southampton v Bournemouth
Jumatatu Novemba 2
2300 Tottenham v Aston Villa
Tagged with: MICHEZO
Hakuna maoni :