Na Saleh Ally
Nawakumbusha tu
wale wapenda michezo wanaopenda kuwazeesha wachezaji baada ya kitu kidogo tu
kutokea.
Abdi Kassim ‘Babi’ au Michael Ballack wa Unguja alionekana ni ‘Mzee’ na hajiwezi.
Lakini leo zaidi
ya mwaka wa pili anaendelea kuitumikia timu yake ya UiTM ya Malaysia na
anafanya vizuri.
Babi ambaye ni
mtaratibu ndiye nahodha wa timu hiyo ambayo ina wachezaji watatu tu kutoka
Afrika.
Ukiona hata
picha anazopiga na kutupia mtandaoni anaonyesha ni mtu mwenye furaha kubwa
kubwa.
Huenda kupitia
Babi tunaweza kujifunza mambo mengi sana. Kuanzia kwa wachezaji kwamba
hawatakiwi kukata tamaa.
Maana Babi
angekata tamaa, Azam FC ingekuwa ni mwisho wake. Hakukubali ameondoka na hata
kama hachezi ligi kubwa, lakini anacheza soka na anaishi kwa kuingiza kipato
huenda kuliko ambacho angepata Tanzania.
Mabadiliko ya
maisha yanataka ujasiri. Babi ameonyesha na wachezaji wengine wafuate hasa wale
ambao wamekata tamaa umri ukiwa bado unawaruhusu.
Kwa mashabiki,
pia wanapaswa kuachana na tabia ya kuwazeesha na kuwakatisha tamaa wachezaji
wengi wa Kitanzania kwa sababu ya chuki binafsi au kubahatisha mambo.
Watanzania
wengi wameacha kucheza soka au wamekata tamaa wakati wana uwezo. Wameacha hivyo
kwa kuwa tu wamekatishwa tamaa na wao wakakubali kusimamishwa na kushindwa
kuendeleza ndoto zao.
Hakuna maoni :