SIASA

SIASA

MAONI

MAONI

BURUDANI

MICHEZO

/ / CECAFA CHALENJI CUP 2015: UGANDA NA RWANDA KUCHEZA FAINALI


CECAFA2015LEO huko Addis Ababa Nchini Ethiopia, Rwanda na Uganda zimefanikiwa kuingia Fainali ya Kombe la Chalenji baada ya kushinda Mechi zao za Nusu Fainali kwa Mikwaju ya Penati.

Katika Nusu Fainali ya kwanza, Sudan, waliocheza Mtu 10 kuanzia Dakika ya 23 baada ya Bakri Almadina kupewa Kadi Nyekundu, na Rwanda zilitoka 0-0 katika Dakika 90 na Gemu kwenda Nyongeza za Dakika 30 na ndipo Sudan kutangulia kufunga kwa Bao la Atahir Babakir la Dakika ya 100 lakini Rwanda walisawazisha kupitia Jean Baptiste Mugiraneza kwenye Dakika ya 110.

Rwanda walibaki Mtu 10 katika Dakika ya 121 baada ya Isaie Songa kupewa Kadi Nyekundu kwa kumpiga Kipepsi Beki wa Sudan.

Hadi Dakika za Nyongeza 30 kumalizika, Bao zilikuwa 1-1 na ndipo ikaja Mikwaju ya Penati Tano Tano ambazo Rwanda walitoka kidedea kwa Penati 4-2.
Nao Uganda na Wenyeji Ethiopia walicheza Dakika 120 bila kufungana na kisha Uganda kuingia Fainali kwa Penati 5-3.

RATIBA/MATOKEO:
Robo Fainali
Jumatatu Novemba 30
Uganda 2 Malawi 0
Kilimanjaro Stars 1 Sudan 1 [Ethiopia yasonga kwa Penati 4-3]


Jumanne Desemba 1
South Sudan 0 Sudan 0 [Sudan yasonga kwa Penati 5-3]
Rwanda 0 Kenya 0 [Rwanda yasonga kwa Penati 5-3]


Nusu Fainali
Alhamisi Desemba 3
Sudan 1 Rwanda 1 [Sudan yasonga kwa Penati 4-2]

Uganda 0 Ethiopia 0 [Uganda yasonga kwa Penati 5-3]

Jumamosi Desemba 5
Mshindi wa Tatu
Ethiopia v Sudan
Fainali
Uganda v Rwanda

«
Next

Chapisho Jipya

»
Previous

Taarifa za zamani

About Unknown

Asante kwa kutembelea SELASINI HABARI,NITAKUHABARISHA, KUKUELIMISHA NA KUKUBURUDISHA HIVYO USIKOSE KUTEMBELEA SELASINIHABARI.BLOGSPOT.COM.

Hakuna maoni :

Leave a Reply