SIASA

SIASA

MAONI

MAONI

BURUDANI

MICHEZO

/ / SAMATTA AREJEA KAZINI TP MAZEMBE, NI BAADA YA SAFARI YAKE UBELGIJI.



Mshambuliaji Mbwana Samatta, juzi Jumatano amerejea katika klabu yake ya TP Mazembe ya DR Congo, amejikuta katika mazingira mapya baada ya kukabidhiwa kwa kocha wa zamani wa timu ya taifa ya Togo, Hubert Velud.

Velud raia wa Ufaransa ambaye pia aliwahi kuwa kocha wa Paris FC mwaka 1995 mpaka 1999, ambayo kwa sasa inashiriki inashiriki Ligue 2 ya Ufaransa, ametua Mazembe akitokea Klabu ya USM Alger ya Algeria na kuchukua mikoba ya Mfaransa mwenzake Patrice Carteron.

Samatta ambaye alikuwa mbioni kutua Genk ya Ubelgiji, dili lake lilikwama kutokana na mmiliki wa Mazembe, Moise Katumbi kugoma kumuachia.

Meneja wa Samatta, Jamal Kisongo, ameliambia Championi Ijumaa kuwa nyota huyo amerejea katika kituo chake cha kazi ili kuweza kuongeza msukumo wa kuondoka kutokana na Katumbi kutokuwa tayari kupata hasara kutoka kwa straika huyo.

“Samatta tayari amerejea Congo…Hili litasaidia kumpa presha Katumbi ya kumuuza maana hatoweza kukubali apate hasara ya jumla, hivyo atalazimika kukubali matakwa ya mchezaji mwenyewe.


“Lakini pia tumeacha nafasi kwa serikali nayo ione inaweza kutusaidia vipi kwa kuwasiliana na Katumbi ili kuweza kulimaliza jambo hili,” alisema Kisongo.

«
Next

Chapisho Jipya

»
Previous

Taarifa za zamani

About Unknown

Asante kwa kutembelea SELASINI HABARI,NITAKUHABARISHA, KUKUELIMISHA NA KUKUBURUDISHA HIVYO USIKOSE KUTEMBELEA SELASINIHABARI.BLOGSPOT.COM.

Hakuna maoni :

Leave a Reply