SIASA

SIASA

MAONI

MAONI

BURUDANI

MICHEZO

/ / WANACHAMA SIMBA WAIMARISHA ULINZI KAMBI YA SIMBA MJINI SHINYANGA



Wanachama kadhaa wa klabu ya Simba wako mjini Shinyanga kuhakikisha kambi ya kikosi hicho iko salama, salimini.

Wanachama hao pamoja na wanachama wamekuwa wakiweka ulinzi wa kutosha ikiwa ni pamoja na kuhakikisha hakuna figisu au ujanja nje ya uwanja.

Simba inatarajia kushuka dimbani Kambarage mjini Shinyanga, Jumamosi kuwavaa wenyeji wake Stand United.

Kwa kuwa Stand United ni timu ya wanachama, lazima figisu hazikosekani.

Wanachama wa Simba, hasa wale kutoka jijini Dar es Salaam, wanalijua hilo hivyo ambacho wamekuwa wakifanya ni kuhakikisha timu yao iko kwenye usalama

Msemaji wa Simba, Haji Manara amesema hiyo ni moja ya utamaduni wa Simba, wanachama wanahakikisha wapiganaji wao wako salama.

“Wako wanachama kutoka Dar es Salaam, wanashirikiana na wa hapa (Shinyanga). Lengo ni kuona vijana wako salama.

“Ukirudi upande wa wachezaji, kweli wanaendelea vizuri sana na mambo mengine yanaendelea katika mpangilio wake,” alisema Manara.


Simba imekuwa ikishinda mechi zake mfululizo hali iliyoamsha matumaini mapya na wanachama.

«
Next

Chapisho Jipya

»
Previous

Taarifa za zamani

About Unknown

Asante kwa kutembelea SELASINI HABARI,NITAKUHABARISHA, KUKUELIMISHA NA KUKUBURUDISHA HIVYO USIKOSE KUTEMBELEA SELASINIHABARI.BLOGSPOT.COM.

Hakuna maoni :

Leave a Reply