SIASA

SIASA

MAONI

MAONI

BURUDANI

MICHEZO

/ / MSHAMBULIAJI AL AHLY ANAAMINI BADO YANGA WATAWAPA SHIDA MECHI YA MARUDIANO MISRI.

EVOUNA
Straika wa Al Ahly, Malick Evouna, ameshangazwa na jinsi Yanga walivyocheza kwenye mchezo wao wa juzi Jumamosi wa Ligi ya Mabingwa Afrika na kusema kuwa mchezo wao wa marudiano utakuwa mgumu.

Yanga na Al Ahly zilikutana Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa, Dar, kwenye mchezo wa raundi ya pili ya Ligi ya Mabingwa Afrika uliomalizika kwa sare ya 1-1 na zinatarajiwa kurudiana kati ya Aprili 19 na 20.

Mshambuliaji huyo ambaye alicheza mechi hiyo kwa dakika tano akiingia akitokea benchi kuchukua nafasi ya Moamen Zakaria, amesema kuwa kwa muda wote aliokuwa benchi alikuwa akiusoma mchezo huku akishangazwa na Yanga walivyokuwa wakicheza kwa kuonyesha upinzani, tofauti na alivyotarajia. 

Alisema kuwa Yanga wana uwezo mkubwa wa kusonga mbele lakini amebaini kitu kitakachowaangusha ni kutojiamini kwao.

“Mchezo ulikuwa mzuri kwa upande wetu lakini pia nawapongeza Yanga kwa jinsi walivyocheza, wametupa upinzani tofauti na tulivyotarajia.

“Uwezo wa kusonga mbele wanao, hatutawadharau hata kidogo kwenye mchezo ujao, kuna kitu ambacho kinawaangusha, nilipokuwa benchi nilikuwa nawaona wanacheza bila kujiamini, kama watajiamini wanaweza kutufunga,” alisema Evouna.

«
Next

Chapisho Jipya

»
Previous

Taarifa za zamani

About Unknown

Asante kwa kutembelea SELASINI HABARI,NITAKUHABARISHA, KUKUELIMISHA NA KUKUBURUDISHA HIVYO USIKOSE KUTEMBELEA SELASINIHABARI.BLOGSPOT.COM.

Hakuna maoni :

Leave a Reply