SIASA

SIASA

MAONI

MAONI

BURUDANI

MICHEZO

/ / Wakati Tanzania Tukiwa Tunashangilia Kusimamishwa Maofisa TRA, Kenya Wanafanya Hivi.

Kwa wanaofatilia siasa za kenya kulikua na skendo iliyokua inamuhusu waziri wa uhuru Anne Waiguru, huyu Anne Waiguru alikua ni waziri mtu mkubwa na maarufu serikalini.

Zimepotea 795 milion kshs ambazo ni kama 16 billion tz shs amewajibishwa na nyumbani kwake kumepekuliwa na maofisa wa kupambana na rushwa na kukuta mamilioni ya pesa kwenye mabunda, soon atafunguliwa mashtaka na kufungwa.

Juzi hapa Tanzania ufisadi wa escrow umetu cost zaidi 300 billions lakini hakuna hata mmoja aliyepekuliwa na wote wamerudi kua wabunge.

Tunatakiwa kuiga wakenya, sio tunatimua maofisa wa tra na muhimbili alafu tunaanza kujiisifu sana bado tuna safari ndefu kwenye hii vita dhidi ya ufisadi.

Sina nia ya kubeza anachofanya Magufuli, nampongeza ila tunapaswa kushinikiza yafanyike zaidi ya hapa na tumuunge mkono.


Kenya wana upinzani imara ndio maana kukitokea ubadhirifu kidogo tu wanaibana serikali hadi inawachukulia hatua wahusika.

Tusiwabeze wapinzani wa serikali tuwasapoti maana wao ndio wanaweza kuibana serikali kwa niaba yetu panapofanyika madudu kama haya

«
Next

Chapisho Jipya

»
Previous

Taarifa za zamani

About Unknown

Asante kwa kutembelea SELASINI HABARI,NITAKUHABARISHA, KUKUELIMISHA NA KUKUBURUDISHA HIVYO USIKOSE KUTEMBELEA SELASINIHABARI.BLOGSPOT.COM.

Hakuna maoni :

Leave a Reply